돌나라 Doalnara

[스와힐리어] 틀림없는 天國의 주인들 Wamiliki Bayana wa Mbingun 본문

PD수첩과 jtbc 방송에 대한 돌나라 입장-돌나라 석선 선생님 말씀

[스와힐리어] 틀림없는 天國의 주인들 Wamiliki Bayana wa Mbingun

돌나라 2022. 12. 14. 09:45

 

[Wamiliki Bayana wa Mbinguni]

 

Wakati wowote maadui wanapoinuka kunipiga, Mimi huchukua muda na kujitafakari. Je, hakika Mimi ni Mwana wa Mungu wa kweli? Au, je, Mimi ni kiongozi wa dini ambaye anawadanganya watu wa kuhurumiwa na kuwaongoza wote kwenye kifo chao? Huwa Ninajichunguza Mara kwa mara. Walakini, haijalishi ni kiasi gani Ninajichunguza , Bila shaka Mimi ni Mwana wa Mungu. Na ndiyo sababu ninaweza kusema kwa ujasiri, na nina uhakika sana.

Kwa hivyo watu hawa wasio na waa ni akina nani? Je, ni Doalnara ? Au ni mtu mwingine? Basi wacha tuangale Doalnara kwanza. Hebu tuangalie na tuone kama ni wao kweli, hatua kwa hatua.

 

1. Wananchi wa Doalnara ni watu wanaotii Neno la Mungu 100%.

2. Wananchi wa Doalnara ni watu wanaoziweka Amri Kumi kwa maisha yao yote.

3. Wananchi wa Doalnara ni watu ambao wametupilia mbali ulafi na ubinafsi.

4. Wananchi wa Doalnara ni watu wasio na ubinafsi ambao wametupilia mbali ubinafsi.

5. Wananchi wa Doalnara ni watoto halisi wa Mungu wanaomtumikia na kumheshimu Mungu kama Baba yao Halisi na Mama yao Halisi.

6. Wananchi wa Doalnara hawana udanganyifu vinywani mwao, wana tabia zisizo na mawaa, na hata hawatendi dhambi katika mawazo yao.

7. Wananchi wa Doalnara hawali vyakula vichafu -- nguruwe, nyama ya ng'ombe, nyama ya mbwa, na hata samaki -- na wanakula tu vyakula safi, vya asili, chakula cha bustani ya Edeni.

8. Wananchi wa Doalnara wanapofanya ukulima , hawatumii kemikali hatari au mbolea. Wanakula tu nafaka na mboga safi zinazolimwa na Mbingu.

9. Kwa sababu wananchi wa Doalnara wote ni watu wema, hakuna uzio katika ujiranii wanakoishi, na hawafungi milango yao. Ndio maana nchi ulimwenguni huwa wanasema "Jamii Isiyo na Uhalifu" katika ujirani wao.

10. Ingawa wanaishi kama majirani kwa miongo mingi, hakuna ugomvi; ni watu wapole na wenye amani daima, watu wazuri ambao huimba nyimbo za shukrani kila mara.

11. Wananchi wa Doalnara ni wana na mabinti wazuri ambao huwatendea wazazi wao wa dunia, wa kimwili kama miungu wanaoonekana na wanaonyesha uchaji kabisa kwao, na wanawapenda sana Wazazi wa mbinguni na wanawatumikia kwa uchaji kabisa.

12. Ndiyo maana ingawa Wazazi wa Mbinguni wana idadi isiyohesabika ya watoto katika malimwengu na katika galaksi zingine, Wanaishi na watoto hawa wa uchaji milele.

13. Pia, watoto hawa wa dunia wana moyo ambao ndugu wakubwa katika malimwengu na galaksi zingine hawakuwahi kuwa nao, na wameinuka kwa uthabiti na hasira isiyoweza kuvumilika ili walipize kisasi kwa adui wa Mzazi wao.

14. Kwa maisha yao yote, watoto hawa wamelia mchana na usiku ili kuondoa kinyongo cha Wazazi wa mbinguni.

15. Mwishowe, wao ndio watoto pekee waaminifu katika malimwengu wanaowatetea Wazazi Halisi kutokana na mashtaka yote ya aibu, ya uwongo na kuwatukuza mbele ya mataifa ya malimwengu.

16. Watoto hawa wanastahili pongezi sana hivi kwamba Wazazi wa Mbinguni wanawashukuru kwa machozi.

17. Ndiyo maana Wazazi wa Mbinguni wamewapa watoto hawa pekee kile ambacho hakijawahi kutolewa kihistoria kwa watu wengine wowote katika kipindi cha miaka elfu sita iliyopita, au kwa kiumbe yeyote wa mbinguni: Amri Kumi, Amri Kumi Fahamivu, Amri Kumi za dhahabu.

18. Wazazi wa Mbinguni watawapandisha watoto hawa wapate kuwa wazaliwa wa kwanza wa malimwengu, na Watajadili mambo yote ya malimwengu pamoja nao na kutimiza majaliwa yote ya malimwengu pamoja nao.

19. Wazazi wa Mbinguni na hawa wazaliwa wa kwanza wa Doalnara ni wamoja, hawawezi kutenganishwa milele. Wataishi kwa furaha milele kama familia moja.

20. Watoto hawa ndio pekee ambao wametimiza kikamilifu [masharti ya uzima wa milele].

21. Kwa hivyo, kando na watoto hawa, hakuna mtu mwingine wa kumpa malimwengu kama urithi. Anatoa mbingu ya milele, ya malimwengu kama urithi kwa watoto hawa wapendwa wa Torati, na anaishi pamoja nao.

 

[Lakini mwisho, watu watakatifu wa Aliye Juu Zaidi watapewa ufalme, nao watatawala milele na milele.]

 

 

Comments